Msongo wa mawazo unaweza kukupelekea ushindwe kufanya shughuli zako za
kila siku kwa ufanisi zaidi,kukufanya kupoteza hamu ya kula. Jambo la kufurahisha ni kuwa msongo wa mawazo unaepukika, leo nimejaribu kueleza baadhi ya mambo ambayo yanaweza kukuwezesha
kuepukana kupata msongo wa mawazo.
jizoeze kukabiliana na changamoto za maisha
Katika maisha huwa tunakutana na mambo ambayo hatukutaka kukutana
nayo na pia tunashindwa kupata yale tuliyoyataka, karibu kila mtu huwa
anapitia hali hii kwa namna moja au nyingine. Jifunze kukabili
changamoto na sio kusikitika kwa nini mambo hayajawa kama ulivyotaka na
kubaki ukisononeka. Jaribu kukubali mambo kwa busara zaidi, na utulivu
huku ukitafakari nini cha kufanya ili kulipata lile ulilo kusudia.
Changamoto iwe ni chachu ya wewe kuzidi kukazana na kujaribu zaidi
Usiwaze zaidi au usikae na jambo linalo kusumbua moyoni
Pale unapokutana na jambo ambalo umeshindwa kulitatua ni vyema
ukamshirikisha mzazi wako au mlezi, rafiki wa karibu, mume au hata
mshauri. Jifunze kutokuweka mambo yanayokuumiza moyoni maana katika hali
hiyo ni rahisi sana kupata msongo wa mawazo. Uwe na tabia ya kupeleka
wasiwasi na hofu zako zote mbele za Mungu kwa maombi na pia kuongea na
mtu ambaye unajua atakuwa msaada kwako
Jali afya yako kiujumla
mara nyingi tunakuwa na shughuli nyingi kiasi cha kuusahau mwili na
kuuchukulia tu kwa juu juu. Ni muhimu sana mwili wako uwe katika hali
nzuri na afya bora ili uweze kufanya kazi zako vizuri na kwa wepesi.
Hakikisha unakula chakula chenye virutubisho bora na pia unakunywa maji
ya kutosha. Fanya mazoezi ya viungo mara kwa mara na pata muda wa
kutosha wa kupumzika kila siku.
Pangilia mambo yako vizuri
hakikisha unapangilia mambo yako na shughuli zako za kila siku,hii itakusaidia sana kuepukana na msongo mawazo ,ni muhimu kuishi kwa mpangilio ,panga maisha yako vizuri usiishi au usiongozwi na matukio
jaribu kufanya mazoezi kula matunda
hii itauweka mwili wako vizuri na kukuepusha na msongo mawazo ,faida za matoezi tembelea link hii hapahizi ni faida za kufanya mazoezi uboreshe afya na maisha yako
mungu awabariki wote!!!!!!
No comments:
Post a Comment