welcome Youth in your blogs that offer free knowledge about life ,welcome to learn,to share
Thursday, 26 November 2015
Friday, 13 November 2015
This Is How You Can Develop A Highly Successful Mind
SOMA ZAIDI KWA KU CLICK HAPAUBONGO WENYE MAFANIKIO
How To Be Successful In Life: 13 Tips From The World’s Most Successful People
No matter how old you are, where you’re
from or what you do for a living, we all share something in common—a
desire to be successful. Each person’s definition of success is
different, however, as some may define success as being a loving and
faithful spouse or a caring and responsible parent, while most people
would equate success with wealth, fame, and power.
We all want to achieve success so we
could live a comfortable life—have financial freedom, drive a nice car,
and live in a beautiful house. However, although success can be
achieved, it does not come easy.
There are a lot of tips and strategies out there on how to be successful in life,
but I am still a firm believer that there is no better way to succeed
than to follow that footsteps of those who have already done so. Here
are 13 success tips from some of the world’s most successful and
renowned people:
1.THINK BIG

From Michelangelo Buonarroti, Great Renaissance Artist: “The
greater danger for most of us lies not in setting our aim too high and
falling short; but in setting our aim too low, and achieving our mark.”
2.Find what you love to do and do it.
From Oprah Winfrey, Media Mogul: “You know you are on the road to success if you would do your job and not be paid for it.”
3. Learn how to balance life.
From Phil Knight, CEO of Nike Inc.: “There
is an immutable conflict at work in life and in business, a constant
battle between peace and chaos. Neither can be mastered, but both can be
influenced. How you go about that is the key to success.”
4. Do not be afraid of failure.
From Henry Ford, Founder of Ford Motors: “Failure is simply the opportunity to begin again, this time more intelligently.”
5. Have an unwavering resolution to succeed.
From Colonel Sanders, Founder of KFC: “I
made a resolve then that I was going to amount to something if I could.
And no hours, nor amount of labor, nor amount of money would deter me
from giving the best that there was in me. And I have done that ever
since, and I win by it. I know.”
6. Be a man of action.
From Leonardo da Vinci, Renaissance Genius :“It
had long since come to my attention that people of accomplishment
rarely sat back and let things happen to them. They went out and
happened to things.”
7. Avoid conflicts.
From Theodore Roosevelt, 26th President of America: “The most important single ingredient in the formula of success is knowing how to get along with people.”
8. Don’t be afraid of introducing new ideas.
From Mark Twain, Famed Author: “A person with a new idea is a crank until the idea succeeds.”
9. Believe in your capacity to succeed.
From Walter Disney, Founder of Walt Disney Company: “If you can dream it, you can do it.”
10. Always maintain a positive mental attitude.
From Thomas Jefferson, 3rd President of America: “Nothing
can stop the man with the right mental attitude from achieving his
goal; nothing on earth can help the man with the wrong mental attitude.”
11. Don’t let discouragement stop you from pressing on.
From Abraham Lincoln, 16th President of America: “Let no feeling of discouragement prey upon you, and in the end you are sure to succeed.”
12. Be willing to work hard.
From JC Penny, Founder of JC Penney Inc.: “Unless
you are willing to drench yourself in your work beyond the capacity of
the average man, you are just not cut out for positions at the top.”
13. Be brave enough to follow your intuition.
From Steve Jobs, Co-founder of Apple Inc.: “Have
the courage to follow your heart and intuition. They somehow already
know what you truly want to become. Everything else is secondary.”
DO YOU LIKE IT COMMENTS,SHARE OR LIKE....
UNGANA NA MSHAURI WA MASUALA YA UCHUMI DUNIANI
click hapaPAUL ZIEGLER FINANCIAL ADVISOR
MTEJA NI MFALME,MKARIBISHE VYEMA..........!!!!!!!
Wateja ni msingi wa biashara, umeshawahi kujiuliza je biashara inaweza kwenda bila wateja? Bila wateja wa kuwauzia bidhaa au kutoa huduma biashara haiwezi kuwepo. Wajasiriamali wanahangaika na biashara zao kwakuwa wanaamini watapata wateja.
Wateja ni kila kitu katika biashara. Hospitali, vyuo, hoteli, daladala, magazeti, radio na biashara mbalimbali unazozifahamu zote zinahitaji wateja ili ziweze kuendelea. Ukosefu wa uelewa kuhusu wateja ni moja ya sababu zinazofanya biashara zianguke na kufungwa baada ya kuanzishwa.
Pamoja na changamoto katika soko bado wajasiriamali wanashindwa kuelewa ni kwa namna gani wanaweza kukidhi mahitaji ya wateja wao.
. Fanya utafiti wa mahali pazuri pa kufanyia biashara.
Eneo ambalo biashara ipo ni jambo la msingi sana katika kuwavutia wateja na kujenga ufanisi katika biashara. Ni vyema pia kutambua si kila biashara inafaa kwa kila eneo na vilevile si kila eneo linafaa kwa kila biashara!
Unaweza kulalamika kwamba biashara sio nzuri na mambo hayaendi lakini kumbe mwanzo wa yote ni biashara yenyewe kutokuwa kwenye eneo sahihi, haya ni makosa yanayofanywa na wajasiriamali wengi hivyo chagua eneo sahihi kwaajili biashara yako.
Inawezekana upatikanaji wa maeneo ya biashara hasa maeneo mazuri yanahusisha gharama kubwa katika upatikanaji wake, ni muhimu ufanye tathmini ya uhusiano wa eneo na aina ya biashara unayotegemea kufanya.
. Tambua wateja halisi wa biashara yako.
Je ni wapita njia? Unapoamua kufanya biashara fikiria pia juu ya walengwa halisi wa biashara husika, ingawa wanaweza kutokea wateja mbalimbali lakini lazima walengwa wawepo.
Elewa wateja ni msingi wa mafanikio katika biashara yako, jiulize wateja wako ni akina nani, nini kitawasukuma kuja kununua kwako, je ni watu wenye uwezo wa kifedha kwa kiasi gani na wanatoka wapi? Ukijiuliza maswali haya utaweza kufahamu namna ya kubuni biashara nzuri kwaajili ya wateja wako.
Kwa mfano ukienda benki kuna akaunti za aina mbalimbali kutokana na madaraja ya wateja, kuna akaunti za makampuni, akaunti za watoto n.k. Hivi ndivyo na wewe kama mjasiriamali unatakiwa kufikiria kuhusu aina ya wateja wako.
Ni muhimu kuwa na mchanganuo wa aina mbalimbali za wateja unaowalenga katika bishara yako. Haiwezekani ‘’nguo’’ moja ikamtosha kila mtu! Kwa mfano kama umeamua kufungua duka la nguo jiulize walengwa ni kina nani na utawapataje?
Kumbuka soko ni kubwa sana na wateja ni wengi, hivyo wewe kama mjasiriamali unatakiwa kuwaainisha wateja wako katika matabaka kutokana na aidha mila, desturi, uwezo wa kiuchumi, jinsia, elimu, au maeneo wanayotoka.
. Ainisha bei stahiki ya bidhaa zako.
Ni muhimu kwa mjasiriamali kupanga bei za bidhaa zake kwa namna ambayo itawaridhisha wateja. Pamoja na kuwa na soko la bidhaa zako, yakupasa kuwa na bei zenye kukubalika miongoni mwa wateja wako.
Vilevile angalia uwezo wa kiuchumi wa eneo husika, zipo baadhi ya bidhaa ambazo bei zake zinaeleweka na zipo bidhaa ambazo bei zake hutofautiana kutokana na mahali. Hii yote inatokana na uwiano wa kiuchumi, mila, desturi na tamaduni za jamii husika.
Ni muhimu kuelewa na kukumbuka kuwa wewe kama mjasiriamali una wajibu wa kuwatafuta wateja, kuhakikisha wanakuja kwako na si wateja wakutafute wewe. Wapo wajasiriamali baada ya kuanzisha biashara wanakaa kusubiri waje badala ya kuwatafuta
. Wafahamu washindani wako.
Tafuta namna ya kuwafahamu washindani wako kujua wanafanya nini kukidhi mahitaji ya wateja wao, ni muhimu kujifunza mabaya na mazuri ya washindani wako bila kuwachukulia washindani wako kama maadui.
Ni busara mara kwa mara ujiulize ni mahali gani kwingine wateja wako wanapoweza kununua bidhaa kama zako unazouza? Ni muhimu kufanya hivyo kwasababu wateja wengi hupenda kwenda mahali penye unafuu kupata bidhaa wanazohitaji na wapo tayari kwenda popote.
Pamoja na kuwafahamu washindani wako yakupasa kama mjasiriamali kuwa tofauti na washindani wako. Kuwa mbunifu kwa kutafuta namna ambayo itaweza kukutofautisha na washindani wako hata kama wote mnauza bidhaa zinazofanana.
Kuna namna mbalimbali ambazo unaweza kujitofautisha na washindani kama vile utoaji wa punguzo la bei kwa wateja wanaonunua bidhaa kwa kiasi kikubwa, utayari wa kupeleka bidhaa hadi eneo husika la mteja na njia nyinginezo.
. Biashara ni matangazo, jinadi kwa watu.
Je biashara yako inafahamikaje kwa watu? Tafuta namna mbalimbali zenye gharama nafuu ili kuweza kufikisha ujumbe wa kile unachokifanya. Mfano jaribu kuweka matangazo madogo madogo ya biashara yako kwenye magazeti, majarida na mabango makubwa ya biashara mbalimbali. Mbinu hii ya kutangaza biashara imewasaidia wengi kupata wateja wengi katika biashara zao.
. Fanya tathmini ya biashara yako.
Ni vizuri kujiuliza maswali kama vile, je una wastani wa wateja wangapi kwa siku, juma au mwezi? Je unafikiri kuna mwelekeo wa kupata wateja zaidi wa kununua bidhaa zako siku zijazo?
Je wateja wako wapo tayari kununua bidhaa zako kwa bei uliyopanga? Je ni kwa kiasi gani wateja wako wanaridhishwa na huduma unazotoa? Je mahitaji ya bidhaa unazouza yakoje, je ni ya msingi, lazima au ni ya kujifurahisha. Je unaridhia kwa kiasi gani kiwango cha mauzo au mapato yako?
Kama ambavyo tumeweza kuona wateja ni msingi wa biashara yako, wewe kama mjasiriamali jitahidi kufanya lolote linalowezekana uweze kubaki na wateja ulionao, unapofikiria biashara yako fikiria utoaji wa huduma bora, uendeshaji makini wa biashara ili isife kwa kuepuka kupata hasara zinazoepukika, kukuza mtaji na kupanua biashara yako
Nani anasema kujitolea hakulipi na hakuna manufaa?
Wengi wetu tunapenda kushiriki katika kufanikisha jambo fulani kubwa
na hata kujumuika na wenzetu wanaotuzunguka. Kwa jinsi tulivyojifunza
baada ya kukutana na watu wengi wanaojitolea, tunaona kwamba kujitolea
ni namna mojawapo na nzuri zaidi ya kutuwezesha kufanilisha azma hii.
Nani anajitolea?
Kuna aina nyingi tofauti za watu wanaojitolea, wenye misukumo na malengo tofauti. Mtu anayejitolea anaweza kuwa:
Nani anajitolea?
Kuna aina nyingi tofauti za watu wanaojitolea, wenye misukumo na malengo tofauti. Mtu anayejitolea anaweza kuwa:
-
Mtu aliyetambua mahitaji ya jamii yake na kuyashughulikia, anajisikia
kuwajibika kwa jamii, anakwenda hatua mbele zaidi ya majukumu yake ya
msingi.
-
Mtu ambaye anajitolea muda na utaalam wake kwa manufaa ya wengine na wakati huo huo akipiga hatua zaidi mbele.
-
Mtu ambaye halipwi mshahara na hatambuliki kama mwajiriwa
Kujenga ujuzi Kazi ya kujitolea inatoa fursa kwako kujifunza mambo mapya na kupata ujuzi wa kazi pamoja na kujenga hali ya kujiamini. Kefar Mbogela, (28) ni Mratibu Msaidizi wa Mradi, Restless Development. Kefar alianza kujitolea katika asasi hiyo mara baada ya kuhitimu Kidato cha Nne. Baada ya kujitolea kwa miaka mitatu pale Restless Development, hivi sasa ameajiriwa kuratibu mafunzo kuhusu masuala ya Katiba katika mikoa mbalimbali. “Nikiwa chuo kikuu niliwafundisha watu mambo yanayohusu ushiriki wa wananchi. Nimekuwa na ujasiri zaidi na nimepata uzoefu mkubwa katika zoezi hilo, sihitaji tena usimamizi kwa jambo lolote na naweza kushughulika na kundi kubwa tu wakati ninapotoa mafunzo juu ya mambo yanayoigusa nchi yetu.”
Faida za kujitolea
Tunapofi kiria kujitolea, wengi wetu tunafi kiria kufanya kazi bila kupata chochote, hata pesa. Lakini, tunapata mambo mengi na ukweli ni kwamba faida tunazozipata zina thamani zaidi ya fedha!
Kujenga ujuzi
Kazi ya kujitolea inatoa fursa kwako kujifunza mambo mapya na kupata ujuzi wa kazi pamoja na kujenga hali ya kujiamini.
Kefar Mbogela, (28) ni Mratibu Msaidizi wa Mradi, Restless Development. Kefar alianza kujitolea katika asasi hiyo mara baada ya kuhitimu Kidato cha Nne. Baada ya kujitolea kwa miaka mitatu pale Restless Development, hivi sasa ameajiriwa kuratibu mafunzo kuhusu masuala ya Katiba katika mikoa mbalimbali.
“Nikiwa chuo kikuu niliwafundisha watu mambo yanayohusu ushiriki wa wananchi. Nimekuwa na ujasiri zaidi na nimepata uzoefu mkubwa katika zoezi hilo, sihitaji tena usimamizi kwa jambo lolote na naweza kushughulika na kundi kubwa tu wakati ninapotoa mafunzo juu ya mambo yanayoigusa nchi yetu.”
Kujijenga kitaaluma
Kujitolea kunakusaidia katika kujiendeleza kitaaluma – ni fursa ya kunoa ujuzi katika masuala ya uongozi, kujiamini na kujitambua. Utaboresha utendaji wako na mwisho wa siku utapata uzoefu, jambo ambalo linakuongezea uwezekano wa kupata ajira.
Adeline Cosmas, (24), ni Mratibu Msaidizi wa Mradi, Mabinti Tushike Hatamu, mradi unaoishirikisha serikali na asasi za kiraia, unaowalenga wasichana kati ya miaka 10 na 19.
“Nilipokuwa chuo kikuu na mara baada ya kumaliza chuo, nilijitolea katika taasisi ya habari ambapo nilijifunza kufanya kazi na watu wa serikali ya mtaa, hii ilinisaidia nilipoomba kazi.”
Adeline anasema, anamshukuru baba yake ambaye alimfundisha utaalam wake wa kufundisha, aliwafundisha wasichana wa darasa la nne na la tano Kiingereza na Hisabati kwa miezi sita wakati huo akiwa na miaka 19, jambo ambalo lilimjengea moyo wa kuwasaidia wengine.
Kujenga mtandao
Uzoefu unaopatikana kwa kujitolea ni fursa pia ya kujenga mtandao wa marafi ki pamoja na kupata mawazo mapya na mtazamo tofauti wa mambo. Hawa pia ni watu ambao watakumbuka kazi uliyoifanya.
Ridhwan Ridhwan, (26), ni mwalimu wa Arusha School na ni balozi wa Fema ambaye amekuwa akijitolea kama mwelimishaji rika TACAIDS, msimamizi wa mazingira ya shule yake na mtu ambaye amekuwa akizisaidia shule katika mkoa wake kuanzisha klab za Fema. Uzoefu wake umemwezesha kukutana na watu wa kila namna.
“Kwa mitandao niliyoijenga katika shughuli zangu za kujitolea hapa Arusha na wakati nikiwa masomoni, mashirika ya kimataifa kutoka nchi mbalimbali yamekuwa yakinialika katika matukio mbalimbali baada ya kukumbuka kazi ambazo nilizifanya na baadhi ya watu wa mashirika hayo.”
Mwisho wa siku, unapotafakari ulichokifanya – unajisikia vizuri!
KUMBUKA
Jitolee ukiwa na lengo la kusaidia wengine au jamii, badala ya kufi kiria ni namna gani utanufaika kifedha. Unapojitolea, jitume kadri ya uwezo wako kwani huwezi kujua itakusaidiaje hapo baadaye.
SOURCES:Fema 31, uk. 40, na Gaure Mdee
Thursday, 12 November 2015
UNATAKA KUMILIKI BIASHARA? PITA HAPA...
Je, wewe ni mtu mwenye ndoto za kumiliki biashara yako mwenyewe?
Unataka kuwa bosi wewe mwenyewe? Je, ni ngumu? Bila shaka. Changamoto
je? Lazima zitakuwepo. Unahitaji utajiri, elimu na wasifu mrefu? Hapana.
Sasa unafanyaje? Jipange!
Kuendesha biashara yako mwenyewe ni chaguo zuri kikazi na kimaisha.
Inahitaji muda na malengo yako. Anza kwa kutambua kwamba unatakiwa
kujitoa kikamilifu katika kuanzisha kazi yako mpaka itakapokuwa
imesimama imara.
Kuna faida nyingi za kuendesha biashara yako mwenyewe.
✸✸ Uhuru na kubadilika: Uhuru wa kufanya kazi wakati na mahali popote unapotaka. Unaamua kile unachotaka mwenyewe.
✸✸ Fuata ndoto zako: Chagua biashara kulingana na kile unachopenda
kukifanya na ambacho kinaendana na uwezo na ujuzi wako. Kila siku
inakuwa na nafasi mpya ya kukuza uwezo na ujuzi na kufikia malengo yako.
✸✸ Kiwango cha kipato: Kipato unachoingiza kinategemea juhudi zako na
kufanikiwa kwa biashara yako, jambo ambalo si kawaida sana unapokuwa
umeajiriwa.
Si Kazi Ndogo
Yafuatayo ni mambo manne muhimuya kuzingatia ili kuanza biashara:
✸✸ Wazo zuri
✸✸ Maarifa/Uwezo
✸✸ Hamasa na msukumo
✸✸ Rasilimali (za kifedha na zisizo za kifedha)
Wazo zuri
Wazo zuri ni kile kitu ambacho unaweza kukifanya na kupata faida na kufikia uhitaji wa wateja wako.
✸✸ Tambua mahitaji ya watu, ambayo hakuna mtu mwingine anayatoa.
✸✸ Ni bidhaa gani utauza au huduma unayoweza kuitoa vizuri zaidi ya mtu mwingine?
✸✸ Je, bidhaa yako itawashawishi watu kuja kuinunua na kukuletea faida?
✸✸ Fikiria hasara: Unafanya hiyo biashara kutegemea hali ya hewa au unategemea uwezo au maarifa ya watu wengine?
Maarifa na uwezo
Maarifa ni nguvu, hivyo kile unachojua kuhusu biashara yako kitakupa
nguvu kuweza kufanikiwa. Kama mmiliki wa biashara ndogo, unatakiwa kujua
biashara unayotaka kuianzisha; kwa mfano, unataka kuanzisha saluni ya
kukata nywele, lazima uwe unajua jinsi nywele zinavyonyolewa, vifaa gani
vinatumika na kama ikiwezekana wewe mwenyewe ujue jinsi ya kunyoa.
Unaweza kujifunza maarifa haya kwa uzoefu rasmi au usio rasmi, elimu
mafunzo, mazoezi au kujiendeleza kiujuzi. Kama huna maarifa na uwezo
wowote, unapaswa kuhamasishwa ujifunze
Msukumo na hamasa
Una nafasi kubwa ya kufanikiwa kama unalipenda wazo lako na una nia
ya kuliendeleza. Unatakiwa kupenda wazo la biashara unalolifikiria.
Unahitaji nguvu na msukumo kuanzisha na kuendesha biashara. Unatakiwa
uwe tayari kwa ajili ya hasara ambazo unaweza kukumbana nazo.
“Mtazamo wa kijasiriamali unahitajika.” Hii inamaanisha kwamba
utakumbana na changamoto ambazo unatakiwa kuwa tayari kuzikabili, pia
kuna mambo mengine yanakuja kwa kushtukiza. Unapaswa kuzichukulia
changamoto zote kama nafasi ya kutafuta njia ya kutatua nyingine siku
zijazo. Wapo watu wachache wenye bahati ya kufanikiwa chapchap katika
biashara zao, lakini wapo wengi pia ambao huwachukua miaka kuweza kupata
mafanikio kama hayo. Fanya biashara yako kwa bidii, kuwa makini,
jifunze mbinu bora za kutunza fedha, omba msaada na ushauri kutoka
katika vyanzo vya kuaminika.
Rasilimali
Ni muhimu kujua gharama za kuendeleza biashara yako. Unatakiwa kujua
ni shilingi ngapi zinahitajika kupata bidhaa na au kutoa huduma yako.
Bajeti yako lazima ijumuishe gharama za kuanzia, kama vifaa, sehemu ya
kufanyia biashara, kodi na huduma, usafi rishaji wa bidhaa, mishahara ya
wafanyakazi, malipo ya mkopo, ada ya benki, ushuru na kadhalika.
Gharama ikiwa ndogo inakuwa rahisi kuanza.
Kujua gharama ya biashara yako ni muhimu ili kuamua kama inaweza
kukupa faida. Ili biashara ikue, utahitaji kutengeza fedha nyingi zaidi
ya ulizowekeza.
Mipango ya biashara yako
Baada ya kuhakikisha wazo lako, unahitaji kuandaa mpango wa biashara
yako. Huu ni mwongozo unaokuelekeza jinsi ya kulifanyia kazi wazo lako
kwa vitendo. Mipango inajumuisha malengo, mikakati na utendaji.
Andika bajeti
Bajeti yako iwe na makadirio ya mapato na matumizi kwa kipindi cha
angalau miezi sita. Unatakiwa kuandika kiwango cha fedha unachohitaji
kila siku, kila wiki, kila mwezi kuendesha biashara yako. Andika ni
kiasi gani cha fedha kinahitajika kwa gharama zote. Unapoanza biashara
kuwa mkweli. Unaweza usifi kie matarajio yako yote kwa wiki au mwezi wa
kwanza, hivyo unatakiwa kuweka bajeti ya gharama zako hadi uinuke na
kuweza kuiendesha.
Yaliyomo kwenye mipango
Inajumuisha mambo mengi:
Maelezo ya biashara: Nini cha kufanya, kuzalisha au kuuza?
Utafiti wa soko: Ni kina nani unakwenda kuwauzia bidhaa zako au kuwapa huduma?
Uchambuzi wa soko: Kwa nini watanunua bidhaa zako au kufuata
huduma zako? Ni kwa sababu una huduma na bidhaa bora zaidi ya wengine?
Ni sehemu gani nyingine wanaweza kupata huduma hiyo?
Utekelezaji: Utatoaje huduma yako? Wakati gani? Mahali gani? Utawafi kiaje wateja wako?
Changamoto: Ni vikwazo gani vinaweza kujitokeza? Utatuaje? Je, kuna watu ambao wanaweza kukusaidia?
Kutafuta njia ya kupata fedha
Unaweza kuhitaji kuwa na fedha ya kuanzia. Vifutav yo ni vyanzo vinavyoweza kukusaidia.
✸ Akiba yako
✸ Familia
✸ Vyama vya kuweka na kukopa visivyo toa riba
✸ Benki za biasharabila riba
✸ Mikopo midogo ya biashara kutoka kwa watu binafsi
✸ Ruzuku .
SOURES FEMA HIP
KIPI NI BORA KATI YA WAZO LA BIASHARA AU MTAJI???TUNDIKIE MAONI YAKO
Labels:
sources FamaHIP,
UJASIRIA MALI
Location:
Kigoma, Tanzania
Subscribe to:
Posts (Atom)
